Wednesday, November 27, 2013

NDEGE YA MAN UNITED YASHINDWA KUTUA UJERUMANI.

NDEGE iliyobeba kikosi cha Manchester United imelazimika kuahirisha kutua ikiwa mita 400 juu ya barabara wakati wakielekea nchini Ujerumani kwa ajili mchezo wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya dhidi ya Bayer Leverkusen. Hata hivyo ndege hiyo ilitua salama katika jaribio lake la pili katika Uwanja wa Ndege wa Cologne. Klabu hiyo ilikataa kutoa taarifa zozote kuhusiana na tukio hilo. United itafanikiwa kufuzu hatua ya mtoano ya michuano hiyo kama wakifanikiwa kushinda mchezo wao huo utakaochezwa katika uwanja wa Bay Arena.

No comments:

Post a Comment