Wednesday, November 27, 2013

TUNATAKIWA KUMALIZA KAZI SIO KUBWETEKA - WENGER.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amewataka wachezaji wake kutobweteka na kumaliza kazi baada ya kukaribia kuvuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya hatua ya mtoano kwa kuigaragaza Olympique Marseille kwa mabao 2-0. Mabao mawili ya timu hiyo yalifungwa na kiungo mahiri Jack Wilshere katika mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa Emirates na kuifanya Arsenal kufikisha alama 12 katika michezo mitano waliyocheza kwenye kundi F. Arsenal itatakiwa kuepuka kipigo wakati watakapoifuata Napoli nchini Italia kwenye mechi yao ya mwisho itakayochezwa katika uwanja wa San Paolo Desemba 11 mwaka huu. Akihojiwa Wenger amesema ni jambo la ajabu kushindwa kufuzu wakati umefikisha alama 12 lakini ndio ukweli wenyewe hivyo hawapaswi kubweteka kabla hawajamaliza kazi.

No comments:

Post a Comment