Saturday, November 30, 2013

SAMATTA, ULIMWENGU KIBARUANI.

KLABU ya TP Mazembe leo ina kibarua kizito wakati watakapokuwa wenyeji wa timu ya CS Sfaxien ya Tunisia katika fainali ya mkondo wa pili ya Kombe la Shirikisho mchezo ambao utafanyika katika Uwanja wa Mazembe jijini Lubumbashi. Mazembe watatakiwa kushinda mabao 3-0 ili kuhakikisha wanatwaa taji hilo baada ya kufungwa mabao 2-0 katika fainali ya mkondo wa kwanza iliyofanyika katika Uwanja wa Olympique de Rades jijini Tunis wiki iliyopita. Hiyo itakuwa nafasi ya kipekee kwa wachezaji nyota wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaocheza katika klabu hiyo kuandika historia ya kuvaa medali katika michuano mikubwa kabisa barani Afrika. Bingwa katika michuano hiyo ataibuka na kitita cha dola za kimarekani 625,000 wakati mshindi wa pili atachukua dola 432,000.

No comments:

Post a Comment