Monday, December 23, 2013

BLANC AWAHIMIZA WACHEZAJI WAKE KUTOMTEGEMEA MOJA KWA MOJA IBRAHIMOVIC.

MENEJA wa klabu ya Paris Saint-Germain, Laurent Blanc ameonya kikosi chake kuwa kinatakiwa kuwa makini wanapokuwa mwa adui baada ya kutoka sare ya kufungana mabao 2-2 na Lille. Blanc pia amedai kuwa wahezaji wake hawapaswi kumtegemea moja kwa moja mshambuliaji nyota wa klabu hiyo Zlatan Ibrahimovic. Ibrahimovic alifunga bao la kuongoza kwa timu yake dakika ya 27 lakini Lille walikuja juu na kurudisha bao hilo kupitia kwa Rio Mavuba kabla ya Salomon Kalou hajaongeza lingine huku PSG wakisawazisha kupitia bao la kujifunga la Marko Basa na kupelekea timu hizo kugawana alama moja kila mmoja. Mara baada ya mchezo huo Blanc alikitaka kikosi chake kutowategemea sana Ibrahimovic na Edinson Cavani ambaye alikosa mchezo huo kwasababu binafsi. Blanc amesema pamoja na kufurahishwa na kiwango bora walichokionyesha lakini matokeo hayakumridhisha kwasababu kuna nafasi nyingi walizokosa ambazo kama wangezitumia vyema wangeweza kuibuka na ushindi katika mchezo huo. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa wachezaji wote wanatakiwa kuwa makini pindi wafikapo langoni mwa adui na sio kuwategemea moja kwa moja Ibrahimovic na Cavani.

No comments:

Post a Comment