Monday, December 23, 2013

RIBERY APEWA TUZO NYINGINE NCHINI UJERUMANI.

IKIWA ni chini ya saa 24 baada ya kutajwa kama mchezaji bora wa michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia, Franck Ribery kwa mara nyingine ametajwa kama mchezaji bora wa mwaka nchini Ujerumani. Baada ya pia kushinda tuzo hiyo mwaka 2008, gazeti maarufu la michezo la Ujarumani, Kicker lilimpigia nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa kuwa mchezaji bora wa mwaka kutokana na kiwango alichokionyesha kiwa na Bayern Munich. Ribery anaungana na washindi wengine waliowahi kunyakuwa tuzo hiyo akiwemo kocha wa Borussia Dortmund Jurgen Klopp mwaka 2012 na kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani Joachim Loew mwaka 2011. Jmamosi iliyopita Ribery mwenye umri wa miaka 30 alichukua tuzo ya mchezaji bora wa michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia baada ya Bayern kuwagaragaza wenyeji kwa Raja Casablanca kwa mabao 2-0 jijini Marrakech na kufanyiwa kunyakuwa taji la nne kwa mwaka huu. Ribery amekuwa mchezaji munimu kwa Bayern kuwa timu ya kwanza ya Ujerumani kushinda mataji matatu likiwemo la Ligi ya Mabingwa, Bundesliga, Kombe la Ujerumani sambamba na UEFA Super Cup.

No comments:

Post a Comment