Sunday, December 22, 2013

TUNAHITAJI MAPUMZIKO - KLOPP.

MENEJA wa klabu ya Borussia Dortmund, Jurgen Klopp amekiri kuwa kikosi chake kinahitaji mapumziko ya majira ya baridi baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka Hertha Barlin jana. Dortmund wamekuwa wakisumbuliwa na majeruhi katika mzunguko wa kwanza wa ligi msimu huu ambapo sasa wako nyuma ya vinara wa Bundesliga Bayerm Munich kwa alama 12. Kipigo hicho cha jana walichopata nyumbani kinakuwa cha tatu mfululizo na Klopp sasa anajipanga kurejesha makali ya timu yake ambayo yamepotea kutokana na majeruhi ya wachezaji yaliyomwandama. Klopp amekiri kuwa wanahitaji mapumziko ili kujipanga na kuangalia mapungufu yao ili waweze kurejea katika kiwango chao.


No comments:

Post a Comment