Sunday, December 22, 2013

HAKUNA WA KUIFUNGA ARGENTINA KATIKA MAKUNDI YA KOMBE LA DUNIA - MARADONA.

NGULI wa soka wa Argentina, Diego Armando Maradona ametamba kuwa hakuna nchi yoyote katika kundi lao itakayoweza kuizuia timu ya taifa ya nchi hiyo kusonga mbele katika michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil mwakani. Argentina imepangwa katika kundi F sambamba na nchi za Nigeria, Iran na Bosnia-Herzegovina ambapo nchi hiyo itacheza mechi yake ya ufunguzi dhidi ya Nigeria Juni 25. Maradona amesema sio Nigeria ambao ni mabingwa wa soka barani Afrika wala nchi nyingine yoyote waliopangwa nayo inayoweza kuwazuia kusonga mbele. Nguli huyo aliendelea kudai kuwa Argentina itafanikiwa kunyakuwa taji lake la tatu nchini Brazil ingawa amesema itakabiliwa na vikwazo kutoka kwa nchi za Ujerumani, Uholanzi na wenyeji wa michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment