Sunday, December 22, 2013

PELLEGRINI AMUOGOPA SUAREZ.

MENEJA wa klabu ya Manchester City, Manuel Pellegrini amekiri kuwa kikosi chake kitakabiliwa na wakati mgumu kumdhibiti Luis Suarez wakati watakapocheza na Liverpool Alhamisi. City wamekwea mpaka katika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu wakiwa nyuma ya Liverpool kwa alama moja baada ya ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Fulham ambao umewafanya kufikisha ushindi mechi nane kati ya tisa walizocheza katika mashindano yote. Hata hivyo safari ya City kuelekea Anfield itawakutanisha na Suarez ambaye yuko katika kiwango cha juu katika upachikaji mabao akiwa ameshafunga mabao 10 katika mechi nne zilizopita na kumfanya kufikisha jumla ya mabao 19 katika mechi 12 za ligi alizocheza. Pellegrini amesema mchezo wao dhidi Liverpool utakuwa mgumu haswa ukizingatia Suarez yko katika kiwango cha juu kabisa hivi sasa.

No comments:

Post a Comment