Sunday, December 22, 2013

LIVERPOOL INAWEZA KUTISHA ZAIDI - RODGERS.

MENEJA wa klabu ya Liverpool, Brendan Rodgers anafikiri kikosi chake kinaweza kucheza kwa kiwango cha juu zaidi baada ya kuigaragaza Cardiff City kwa mabao 3-1 na kuweka hai matumaini yao ya kunyakuwa taji la Ligi Kuu nchini Uingereza. Mabao mawili yaliyofungwa na Luis Suarez na kumfanya kufikisha mabao 19 katika ligi msimu huu umeifanya Liverpool kupata ushindi wake wa nne na kuwapeleka kileleni mwa msimamo wa ligi. Rodgers anaamini kikosi chake kinaweza kunyakuwa taji la kwanza la ligi toka mwaka 1990. Kocha huyo amesema kikosi chake kilionyesha kiwango bora katika mchezo dhidi ya Cardiff lakini akatamba bado kuna nafasi ya kuboresha kiwango chao zaidi ya hapo.

No comments:

Post a Comment