Sunday, December 22, 2013

MOURINHO AMGWAYA OZIL.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amesifu kiwango cha Mesut Ozil toka atue katika Ligi Kuu nchini Uingereza na kudai kuwa ndio kitu klabu ya Arsenal ilikuwa inakikosa ili inyakue taji la ligi. Nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani alitua Arsenal kwa ada ya euro milioni 50 na mpaka sasa ameshafunga mabao manne na kutoa pasi za mwisho saba. Mourinho ambaye amefanya kazi na Ozil kwa miaka mitatu akiwa Real Madrid anafikiri kiungo huyo akiwa sambamba na Aaron Ramsey na Theo Walcott wanaweza kuingoza Arsenal kuwanyakuwa taji. Kocha huyo amesema Ozil ni mmoja wa wachezaji ambaye unamnunua ili aje kuziba pengo katika timu yako na haitaji muda wa kuzoea mazingira kwasababu ni mchezaji aliyekamilika.

No comments:

Post a Comment