Monday, December 23, 2013

RONALDO SASA WATATU KWA KUPACHIKA MABAO MADRID.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo sasa kuna wachezaji watatu pekee mbele yake katika orodha ya wachezaji waliofunga mabao mengi zaidi baada ya kufunga bao katika mchezo dhidi ya Valencia jana. Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno amefunga mabao 164 katika mechi 151 na kufikia rekodi ya mshambuliaji wa kimataifa wa Mexico Hugo Sanchez ambaye alifunga mabao 164 katika mechi 207 alizochezea Madrid. Ronaldo sasa amezidiwa na Santillana aliyefunga mabao 186, Alfredo de Stephano aliyefunga mabao 216 na Raul anayeongoza orodha hiyo kwa kufunga mabao 228. Katika mchezo wa jana Madrid walifanikiwa kuinga Valencia kwa mabao 3-2.

No comments:

Post a Comment