Monday, December 23, 2013

VAN GAAL AITAMANI TOTTENHAM HOTSPURS.

KOCHA wa timu ya taifa ya Uholanzi, Louis van Gaal amedokeza nia yake ya kuinoa klabu ya Tottenham Hotspurs lakini mpaka baada ya michuano ya Kombe la Dunia 2014. Tim Sherwood ndio amepewa mikoba ya kuinoa kwa muda Tottenham akichukua mikoba ya Andres Villas-Boas lakini kocha huyo amesisitiza kuwa anataka kibarua cha moja kwa moja baada ya kupata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Southampton. Van Gaal ambaye amewahi kuzinoa Barcelona na Bayerm Munich kwasasa ana mkataba na Uholanzi unaomalizika Julai mwakani lakini amekataa kukubali kunoa timu mbili kwa wakati mmoja. Kocha huyo amesema ni kweli anapenda kufanya kazi katika Ligi Kuu nchini Uingereza lakini hawezi kufanya kazi mbili kwa wakati mmoja hivyo muda wake wa kuondoka Uholanzi utakapofika na bado nafasi ikiwa wazi hakuna shaka kwamba lazima ataomba.

No comments:

Post a Comment