Friday, December 20, 2013

ITAKUWA HESHIMA KUBWA KWANGU KAMA TOTTENHAM WAKINIHITAJI - DE BOER.

MENEJA wa klabu ya Ajax Amsterdam ya Uholanzi, Frank de Boer amesema itakuwa ni jambo la heshima kwake kuhusishwa na nafasi ya umeneja iliyokuwa wazi katika klabu ya Tottenham Hotspurs. Spurs imekuwa bila kocha toka imtimue Andres Villas-Boas Jumatatu iliyopita na nafasi yake kuachiwa kocha wa muda Tim Sherwood ambaye alishindwa kukiongoza kikosi hicho ipasavyo na kujikuta wakitolewa katika Kombe la Ligi kwa kufungwa na West Ham United kwa mabao 2-1. De Boer amesema kama Spurs wanamhitaji ni heshima kwake lakini kwasasa anaelekeza nguvu zake katika klabu yake ya Ajax. Mapema Alhamisi wakati wa kocha huyo, Guido Albers alibainihsa kuwa De Boer ambaye ni mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Uholanzi amekuwa akiitaka nafasi ya Villas-Boas ingawa Spurs wenye wenye hawajamfuata rasmi.

No comments:

Post a Comment