Friday, December 20, 2013

SITAJALI KAMA RONALDO HATAHUDHURIA SHEREHE ZA UTOAJI TUZO ZA BALLON D'OR - RIBERY.

WINGA mahiri wa klabu ya Bayern Munich, Franck Ribery amesisitiza kuwa hatajali kama mshambuliaji nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo atahudhuria au kutohudhuria sherehe za utoaji tuzo ya Ballon d’Or zitakazofanyika jijini Zurich. Kumekuwa na tetsi kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Ureno hatahudhuria sherehe hizo kutokana na mahusiano mabovu na rais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Sepp Blatter lakini Ribery amesema uamuzi wowote utakaochukuliwa na nyota huyo hautamuhusu. Ribery amesema hajawasiliana na Ronaldo na hawajadili naye wala mtu yoyote hivyo hajali kama hatahudhuria sherehe za utoaji tuzo hizo. Baadae Ribery alikiri kuwa uamuzi wa FIFA na Shirikisho la Soka la Ufaransa kusogeza mbele muda wa kupiga kura kwa ajili ya tuzo hiyo unaweza kumnyima nafasi ya kuitwaa kwa mara ya kwanza. Tuzo ya Ballon d’Or ambayo zamani ilikuwa ikijulikana kama tuzo ya mchezaji bora wa dunia wa mwaka inatarajiwa kutolewa Januari 13 mwakani.

No comments:

Post a Comment