Saturday, December 21, 2013

SUAREZ AICHA SOLEMBA ARSENAL BAADA YA KUKUBALI MKATABA MPYA LIVERPOOL.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Liverpool, Luis Suarez amesaini mkataba mpya wa miaka minne kuitumikia klabu hiyo. Suarez mwenye umri wa miaka 26 ambaye alijiunga na Liverpool Januari 2011 amefunga mabao 17 katika 11 za ligi alizocheza msimu huu. Nyota huyo ambaye mkataba wake wa sasa unaishia mwaka 2016 atakunja kitita cha paudi 160,000 mpaka mkataba utakapoisha na baadae kukunja kitita cha paundi 200,000 kwa miaka minne iliyobakia. Suarez amekiri kuwa ukaribu aliokuwa nao na mashabiki wa klabu hiyo ndiyo uliopelekea kufanya uamuzi huo na ni mategemeo yake hatawaangusha katika kipindi atakachokuwepo hapo.

No comments:

Post a Comment