Saturday, December 21, 2013

SEEDORF ATAKUWA KOCHA MZURI KWA MILAN - KAKA.

KIUNGO wa klabu ya AC Milan, Kaka anafikiri kuwa Clarence Seedorf anaweza kuwa kocha mzuri mara atakapoamua kutundika daruga. Kauli hiyo ya Kaka imekuja kufuatia tetesi kuwa Milan imepanga kumchukua Seedorf ili kuziba nafasi ya Massimiliano Allegri mwishoni mwa msimu huu. Kaka ambaye amecheza sambamba na Seedorf kwa miaka sita wakati akiwa Milan anaamini kuwa kiungo huyo abaye kwasasa anacheza klabu ya Botafogo atakuwa mmoja wa makocha bora kabisa duniani siku zijazo. Kaka amesema kila kitu anachofanya Seedorf anafanya kwa uwezo wake na wekedi wa hali ya juu hivyo anadhani atakuwa kocha mzuri ingawa kuna vitu vingi inabidi ajifunze.

No comments:

Post a Comment