Monday, January 27, 2014

BAINES APEWA MKATABA MPYA EVERTON.

KLABU ya Everton imempa mkataba mpya wa miaka minne beki wake mahiri Leighton Baines ambaye alikuwa akinyemelewa na klabu ya Manchester United. Beki huyo wa kimataifa wa Uingereza alikuwa amebakiza miezi 17 kabla ya mkataba wake kumalizika na kulikuwa na tetesi kuwa kocha United David Moyes alikuwa amemuweka katika rada zake. Kocha wa Everton Roberto Martinez alithibitisha kumuongeza mkataba beki huyo na kudai kuwa ni jambo zuri katika kuimarisha kikosi chao. Baines alijiunga na Everton mwaka 2007 na toka kipindi hicho amekuwa sehemu muhimu katika ukuta wa timu hiyo akiwa amecheza mechi 260 mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment