Sunday, January 26, 2014

MESSI HAONDOKI BARCELONA - BABA.

BABA na wakala wa mchezaji nyota wa Barcelona, Lionel Messi kwapamoja wamesisitiza kuwa mshambuliaji huyo hawezi kujiunga na Paris Saint Germain, PSG au klabu nyingine yoyote katika kipindi hiki. Kumekuwa na tetesi kuwa matajiri hao kutoka jiji la Paris walikuwa wamepanga kutenda dau euro milioni 250 litakalovunja rekodi ya dunia kwa ajili ya kumsajili nyota huyo katika kipindi cha usajili majira ya kiangazi. Hata hivyo baba wa mchezaji huyo Jorge Messi amekana tetesi hizo kwamba PSG wanaweza kumuondoa mwanae Camp Noun a kusisitiza hawezi kwenda popote kwasasa. Jorge amesema amesikia tetesi hizo na hajui zilipotokea na kuwahakikishia mashabiki wa Barcelona kuwa Messi bado ni mchezaji wao kwa miaka kadhaa mpaka hapo mkataba wake utakapomalizika mwaka 2018.




No comments:

Post a Comment