Monday, January 27, 2014

ULIKUWA NI UAMUZI MGUMU KUMUUZA MATA - MOURINHO.

MENEJA wa Chelsea, Jose Mourihno amesema ulikuwa ni uamuzi mgumu kumuachia kiungo wa kimataifa wa Hispania Juan Mata kujiunga na mahasimu wao wa Ligi Kuu Manchester United. Mata mwenye umri wa miaka 25 aliondoka Chelsea na kuhamia United kwa ada iliyovunja rekodi ya klabu hiyo. Mourinho amesema meneja kazi ni kutoa maamuzi kama hayo lakini kwa upande wake ulikuwa ni uamuzi mgumu kwasababu bado alikuwa akipenda kubakiwa na nyota huyo katika kikosi chake. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa anapenda kumfurahisha kila lakini ilishindikana kumfurahisha Mata kwasababu alikuwa hampi namba ya moja kwa moja katika kikosi cha kwanza.

No comments:

Post a Comment