Friday, January 24, 2014

FERGUSON AULA UEFA.

RAIS wa Shirikisho la Soka barani Ulaya, UEFA Michel Platini amesema shirikisho hilo limeteua kocha wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson kuwa balozi wa makocha. Ferguson mwenye umri wa miaka 72 ameweka rekodi ya kudumu Old Traford kwa miaka 26 kabla ya kuamua kustaafu msimu uliopita baada ya kushinda mataji 13 ya Ligi Kuu akiwa na klabu hiyo. Akizungumza mara baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji jijini Nyon, Switzerland, Platini amesema Ferguson atakuwa mwenyekiti wa kongamano la makocha linafanyika kila mwaka na pia atakuwa mjumbe wa kamati ya ufundi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa barani humo pamoja na Europa League. Akihojiwa kuhusiana na uteuzi huo Ferguson amesema ni heshima kubwa kwake na anakubaliana na uteuzi huo wa kuwa balozi wa UEFA.

No comments:

Post a Comment