Saturday, January 25, 2014

LI NA BINGWA MPYA WA AUSTRALIA OPEN KWA WANAWAKE.

HATIMAYE mwanadada nyota wa tenisi kutoka China, Li Na ametawadhwa kuwa bingwa mpya wa michuano ya wazi ya Australia kwa wanawake baada ya kumfunga Dominika Cibulkova wa Slovakia katika mchezo wa fainali uliofanyika Katika uwanja wa Rod Laver Arena jijini Melbourne. Li Na ambaye amelikosa taji hilo mara mbili baada ya kufungwa na Kim Cylister katika fainali za mwaka 2011 na Victoria Azarenka mwaka jana, alifanikiwa kunyakuwa taji hilo kwa kumfunga Cibulkova kwa seti mbili bila majibu zenye alama za 7-6 6-0. Akiwa na Umri wa miaka 31, Li Na anakuwa mwanamke mwenye umri mkubwa kushinda taji hilo akivunja rekodi ya Margaret Court ambaye alishinda taji hilo mwaka 1973 akiwa na umri wa miaka 30. Kesho kutakuwa na mchezo mwingine wa fainali ya michuano kwa upande wa wanaume ambapo kinara Rafael Nadal wa Hispania atachuana na Stanislas Wawrinka wa Switzerland.


No comments:

Post a Comment