Friday, January 24, 2014

HAKUNA KINACHISHINDAKANA MBELE ZA MUNGU - FALCAO.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Monaco ya Ufaransa, Radamel Falcao bado hajakata tamaa kuwepo katika michuano ya Kombe la Dunia baadae mwaka huu pamoja na kuumia vibaya goti lake. Nyota huyo wa kimataifa wa Colombia alibebwa na machela kutolewa uwanjani katika mchezo wa Kombe la Ligi nchini Ufaransa ambapo timu yake iliibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Monts d’Or Azergues Jumatano. Klabu hiyo ilithibitisha kuwa nyota huyo aliyevunja rekodiya usajili atafanyiwa upasuaji baada ya vipimo kuonyesha ameumua kwa ndani kwenye goti lake la kushoto. Matumaini ya nyota huyo kucheza michuano ya Kombe la Dunia itakayoanza Juni 12 mwaka huu yanaonekana kutoweka lakini mwenyewe bado hajakata tamaa akidai kuwa anaweza kupona kwa wakati na kushiriki. Falcao amesema akiwajibu mashabiki wake waliokuwa wakimtumia ujumbe wa pole katika mtandao wake wa kijamii wa twitter kuwa mungu anaweza kufanya visivyowezekana vikawezekana nay eye anamuamini.

No comments:

Post a Comment