Sunday, January 26, 2014

MWAMUZI AMEKUWA MKALI SANA DHIDI YA BUFFON - CONTE.

MENEJA wa klabu ya Juventus, Antonio Conte amedai kuwa uamuzi wa kumtoa nje golikipa wa timu hiyo Gianluigi Buffon katika mchezo ulioisha kwa sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Lazio ulikuwa mkali sana. Buffon ambaye ni nahodha wa Juventus alitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumuangusha Miroslav Klose wakati akielekea kufunga na kupelekea mwamuzi Davide Massa pia kuwazaiwadia Lazio penati ambayo ilitiwa kimiani na Antonio Candreva. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Conte mwenye umri wa miaka 44, amesema ni jambo la kusononesha kuwepo kwa sheria kama hiyo kwasababu anadhani penati pekee inatosha bila kuongeza na kadi nyekundu. Pamoja na kuhuzunishwa huko, Conte aliwapongeza wachezaji wake kwa kucheza kwa kujituma na kuhakikisha wanaondoka na walau alama moja baada ya kusawazisha bao huku wakiwa wanacheza pungufu.

No comments:

Post a Comment