Friday, February 21, 2014

BAADA YA KUSHITAKIWA KWA UDANGANYIFU, RAIS WA BARCELONA ASEMA HAWANA CHA KUFICHA KUHUSIANA NA UHAMISHO WA NEYMAR.

RAIS wa klabu ya Barcelona, Josep Maria Bartomeu amesisitiza kuwa hatabadilisha chochote kuhusiana na uhamisho wa Neymar, licha ya utata na mambo ya kisheria yanayotokana na uhamisho huo. Barcelona wameshitakiwa kwa udanganyifu na mahakama ya juu nchini Hispania jana kwa madai ya kukwepa kulipa kodi ya euro milioni 9.1 katika uhamisho wa Neymar kwenda Camp Nou katika majira ya kiangazi mwaka jana. Bartomeu ambaye alichukua nafasi ya Sandro Rosell aliyejiuzulu Januari kufuatia sakata hilo amesema ana uhakika kuwa klabun hiyo itakutwa haina hatia juu ya tuhuma hizo za ukwepaji kodi. Rais huyo amesema mkataba waliosaini na Neymar na klabu ya Santos ulikuwa halali sambamba na mazungumzo, shughuli za kifedha na mengineyo yote yalifanyika kwa mujibu wa sheria hivyo hawana shaka yoyote. Bartomeu aliendelea kudai kuwa watafanya kama walivyofanya mwanzo kama watapewa nafasi ya kumsajili Neymar kwa mara nyingine.

No comments:

Post a Comment