Friday, February 21, 2014

USHINDI DHIDI YA MAN CITY WAMPA JEURI XAVI, ATAMBA BARCELONA KUTOOGOPA TIMU YOYOTE.

KIUNGO mahiri wa klabu ya Barcelona Xavi Hernandez amesisitiza kuwa timu hiyo haimuogopi yoyote katika michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya lakini pia hawatawadharau wapinzani wanaokutana nao. Kauli hiyo ya Xavi imekuja kufuatia ushindi murua wa mabao 2-0 waliopata dhidi ya Manchester City katika mechi ya mkondo wa kwanza hatua ya mtoano ya michuano hiyo ushindi ambao kiungo huyo amesema umewajengea kujiamini zaidi. Xavi amesema hawaogopi timu yoyote lakini hiyo haimaanishi kuwa hawawaheshimu wapinzani wao kama Bayern Munich, Paris Saint-Germain na Atletico Madrid ambao wote wameanza vizuri katika hatua hiyo. Nyota huyo aliendela kusema kuwa kwasasa wako wanacheza katika kiwango kizuri na kila mtu anafurahia kwasababu wanaongoza La Liga, wako katika nafasi nzuri kwenye Ligi ya Mabingwa na pia wamefika fainali ya Kombe la Mfalme.

No comments:

Post a Comment