Thursday, February 27, 2014

BOWE AWAOMBA RADHI MASHABIKI WA LIVERPOOL KWA KAULI YAKE...

BINGWA wa zamani wa masumbwi wa uzito wa juu duniani, Riddick Bowe amewaomba radhi mashabiki wa Liverpool baada ya kuandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter kuwa angependa mashabiki wote wa Liverpool wafe. Bowe raia wa Marekani mwenye umri wa miaka 46, alisukumwa kutuma ujumbe huo baada ya kusumbuliwa na watu wakimtaka kufafanua kwanini ameamua kuwa mshabiki wa Everton. 
Ujumbe huo ulizusha hasira kali kutoka kwa mashabiki wa Liverpool huku wale wa Everton wakimshauri kuwaomba radhi mahasimu wao hao. Bowe aliamua kuandika ujumbe mwingine wa kuomba radhi akidai kuwa amefanya hivyo baada ya kushauri na mashabiki wenzake wa Everton kwakuwa wao ni kitu kimoja.

No comments:

Post a Comment