Friday, February 28, 2014

MAYWEATHER AMENIOGOPA - KHAN.

BINGWA wa zamani wa dunia wa ngumi kutoka Uingereza, Amir Khan amemtuhumu Floyd Mayweather kwa kuchukua chagua rahisi baada ya bondia huyo kukubali kupigana na Marcos Maidana Mei 3 mwaka huu. Khan alishinda kura za katika mtandao baada ya Mayweather mwenye umri wa miaka 36 kuwataka mashabiki wake kuamua bondia wa kupigana naye lakini Mmarekani huyo aliamua kumchagua Maidana raia wa Argentina ambaye ni bingwa wa WBA. Akihojiwa Khan mwenye umri wa miaka 27 amesema anadhani Mayweather amechagua njia rahisi ya kutetea taji lake. Khan amesema ni jambo lililomhuzunisha kwasababu alifuta pambano lake na Devon Alexander lililokuwa lichezwe Desemba mwaka jana kwasababu alikuwa akijua atapigana na Mayweather kwa asilimia 100. Bondia huyo aliendelea kulalama kuwa tayari alishapeleka mkataba na ukasainiwa juu ya pambano lake hivyo akadhani wanaweza kutangaza pambano hilo Desemba, Januari au Februari lakini matokeo yake Mayweather akataka mashabiki kuamua kwa kura. Jambo la kushangaza Khan alishinda katika kura hizo kwa asilimia 57 lakini Mayweather akaamua kupigana na Maidana aliyepata kura chache.

No comments:

Post a Comment