Friday, February 28, 2014

EUROPA LEAGUE YAFIKIA PATAMU.

KLABU za Sevilla na Real Betis zote za Hispania zinatarajiwa kukutana katika hatua ya timu 16 bora katika michuano ya Europa League baada ya kufanikiwa kusonga mbele jana. Baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 katika mechi ya kwanza dhidi ya NK Maribor, Sevilla walihakikisha wanatumia vyema uwanja wao wa nyumbani katika mchezo wa pili na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 hivyo kusonga mbele kwa jumla ya mabao 4-3. Betis wao walisonga mbele baada ya kuigandamiza Rubin Kazan ya Urusi kwa mabao 2-0 hivyo kuwafanya kusinga mbele kwa jumla ya mabao 3-1 kutokana na sare ya bao 1-1 katika mchezo wa kwanza. Kocha wa Napoli Rafael Benitez ambaye alishinda taji hilo akiwa na Chelsea msimu uliopita naye alifanikiwa kusonga mbele baada ya kuiengua Swansea City na ataendelea kutetea taji hilo dhidi ya Porto ambao waliwatoa Wajerumani Eitracht Frankfurt. Tottenham Hotspurs ya Uingereza wao watakwaanza na Benfica ya Ureno katika mzunguko unaofuata huku mabingwa wa Italia Juventus wao wakikwaana na wenzao Fiorentina.

No comments:

Post a Comment