Friday, February 28, 2014

NASRI, ABIDAL WAACHWA UFARANSA.

BEKI wa kati Eric Abidal na kiungo Samir Nasri wameachwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Ufaransa wakati kocha Didier Deschamp alipotaja majina ya wachezaji 24 watakaoiwakilisha nchi hiyo katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Uholanzi utakaochezwa wiki ijayo. Mshambuliaji Antoine Griezmann ni mmoja ya wachezaji walioitwa kwa mara ya kwanza katika kikosi hicho sambamba na beki wa kushoto Lucas Digne ambaye anaziba nafasi ya Gael Clichy wa Manchester City. Griezmann mwenye umri wa miaka 22 anayekipiga Real Sociedad ya Hispania amefunga mabao 19 katika mechi 38 alizochezea timu yake msimu huu. Akihojiwa kama wachezaji hao wameshapoteza namba zao katika kikosi chake Deschamp amesema asingependa kuzungumzia suala hilo lakini anachojua yeye mchezaji muhimu ndio atakayekuwepo katika kikosi chake kitakachokwenda Brazil.

No comments:

Post a Comment