Friday, February 28, 2014

MAPUMZIKO YAMEMUWEKA FITI OZIL - WENGER.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger anaamini mapumziko aliyompa Mesut Ozil yatamsaidia kumrejesha katika kiwango chake na ana uhakika anaweza kuhimili msukumo anaopewa katika timu hiyo. Nyota huyo wa zamani wa Real Madrid alipumzishwa katika mchezo wa ligi dhidi ya Sunderland wiki iliyopita baada ya kukosa penati katika mchezo dhidi ya Bayern Munich kwenye Ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Akihojiwa Wenger amesema huwa hampi msukumo wowote mchezaji huyo kama watu wanavyodai kwasababu huwa anaamini ushindi wa timu unatoka kwa ushirikiano wa wachezaji wote na sio mmoja. Wenger kikubwa anachopenda yeye ni wachezaji wake kufurahia mchezo na kucheza vyema kwa kuelelewana hivyo hana shaka na Ozil kwasababu anapitia kipindi kigumu na kila mtu hupitia huko.

No comments:

Post a Comment