Friday, February 21, 2014

EUROPA LEAGUE YASHIKA KASI.

TIMU za Valencia ya Hispania, Juventus ya Italia na Benfica ya Ureno zimejiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele katika michuano ya Europa League baada ya kushinda mechi zao za mkondo wa kwanza zilizochezwa jana. Kwa upande wa Valencia wao walifanikiwa kuifunga Dynamo Kiev kwa mabao 2-0 katika mchezo ulihamishwa na kuchezwa jijini Nicosia, Cyprus kutokana na vurugu zinazoendelea mji mkuu wa Ukraine, Kiev. Kwa upande wa Juventus na walifanikiwa kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Trabzonspor katika mchezo uliochezwa jijini Turin kuhu Benfica wao wakipaa ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya PAOK Salonika ya Ugiriki. Mechi zingine zilizochezwa jana na matokeo kushangaza ni Ajax Amtserdam ambao walipokea kichapo cha mabao 3-0 nyumbani kwao kutoka kwa FC Salzburg ya Austria huku Porto wao wakilazimishwa sare nyumbani ya mabao 2-2 na Eintracht Frankfurt ya Ujerumani. Kwa upande wa timu za Uingereza mambo hayakuwa mazuri kama ilivyokuwa katika matokeo ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya, ambapo Swansea City walilazimishwa sare ya bila kufungana na Napoli ya Italia huku Tottenham Hotspurs wakichapwa bao 1-0 ugenini na FC Dnipro ya Ukraine.

No comments:

Post a Comment