Friday, February 21, 2014

KLOPP AMTEGEMEA REUS UWANJANI WIKIENDI HII.

MENEJA wa klabu ya Borussia Dortmund, Jurgen Klopp anategemea nyota wake Marco Reus kurejea uwanjani wakati kikosi chake kitakaposafiri kwenda kupambana na Hamburg katika mchezo wa Bundesliga utakaochezwa kesho. Nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani alikosa michezo miwili iliyopita ya Dortmund baada ya kuchanika msuli katika mchezo dhidi ya Werder Bremen uliochezwa mapema mwezi huu lakini anaonekana kuwa fiti kwa ajili ya mchezo huo. Akihojiwa kuhusu afya ya mchezaji huyo Klopp amesema Reus alifanya mazoezi kwa asilimia 100 na alionekana kuwa vizuri hivyo anadhani atakakuwa fiti kwa ajili ya mchezo kesho. Klopp amesema watakwenda katika mchezo huo bila kuwadharau wenyeji wao ambao wanaonekana kusuasua baada ya kufungwa mechi saba mfululizo hatua iliyopelekea kocha wake Bert van Marwijk kutimuliwa na nafasi yake kuchukuliwa na Mirko Slomka.

No comments:

Post a Comment