Friday, February 21, 2014

PUYOL HATIHATI KUCHEZA KOMBE LA DUNIA - GRANDE.

KOCHA msaidizi wa timu ya taifa ya Hispania, Toni Grande amedai kuwa kuna hatihati ya beki wa kati wa klabu ya Barcelona Carles Puyol kuitwa katika kikosi cha nchi hiyo kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Dunia mwaka huu. Kikosi cha Hispania kinachonolewa na Vicente del Bosque kilinyakuwa taji la michuano hiyo miaka minne iliyopita huku kikiwa na safu ya ulinzi imara iliyoongozwa na mkongwe Puyol lakini nyota huyo atakuwa na miaka 36 wakati wa michuano hiyo itakayofanyika nchini Brazil. Kutokana na maswali juu ya afya yake huku akiwa amecheza mechi moja pekee ya La Liga kwa mwaka huu, Grande anafikiri wakati umefika kwa mkongwe huyo kustaafu rasmi soka la kimataifa baada ya kucheza mechi 100. Grande amesema siku zote Puyol amekuwa mchezaji muhimu kwa nchi yake hivyo hawezi kumuondoa moja kwa moja lakini ni suala lililo wazi kuwa anahitaji muda zaidi wa kucheza hususani mechi muhimu za Barcelona.

No comments:

Post a Comment