Thursday, March 6, 2014

AL AHLY YAHAHA KUTAFUTA UWANJA.

KLABU ya Al Ahly ya Misri bado inahaha kutafuta uwanja watakaoutumia kwa ajili ya mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa barani Afrila dhidi ya Yanga huku zikiwa zimesalia siku tatu kabla ya mchezo. Vurugu za mashabiki wao katika mechi ya hivi karibuni imepelekea mamlaka ya nchi hiyo kuifungia timu hiyo kucheza mechi zake katika mji mkuu wa Cairo. Mabingwa hao watetezi wa michuano hiyo hivi sasa wanahaha kujaribu kuomba kutumia uwanja uliopo katika mji wa Alexandria kwa ajili ya mchezo huo lakini muda unaonekana kutokuwa upande kutokana na kubaki siku chache. Mashabiki wa Al Ahly waliwaumiza askari 25 mwezi uliopita wakati wa mchezo wa Super Cup walioshinda dhidi ya CS Sfaxien ya Tunisia katika Uwanja wa Taifa uliopo jijini Cairo. Mamlaka nchini humo inasita kuruhusu mechi yoyote kuchezwa na mashabiki baada ya tukio hilo na kuna uwezekano mchezo huo wa Jumapili ukachezwa bila uwepo wa mashabiki. Al Ahly ilitandikwa bao 1-0 na Yanga katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa michuano hiyo uliochezwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment