Tuesday, March 25, 2014

ARSENAL YAJIPANGA KWA MAISHA BILA WENGER.

KLABU ya Arsenal ikiwa inategemea kocha wake Arsene Wenger kutia saini mkataba mpya lakini tayari wameshaanza kujipanga kuanza maisha bila ya uwepo wa kocha huyo. Wenger ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimi huu tayari ameahidi kuwa ataendelea kuinoa klabu hiyo. Mazungumzo ya mara ya kwanza kuhusiana na mkataba yalikuwa ni kumpa mkataba wa miaka mitatu wenye thamani ya paundi milioni nane kwa mwaka lakini sasa hivi inanekana atapewa mkataba wa miaka miwili pekee. Lakini kipigo cha mabao 6-0 walichopata toka kwa mahasimu wao Chelsea kunaweza kubadili mustakabali wa Wenger huku klabu hiyo ikionyesha kuvutiwa na kocha wa Everton Roberto Martinez na Jurgen Klopp wa Borussia Dortmund kama mbadala wake pindi atakapoamua kuachia ngazi.

No comments:

Post a Comment