Tuesday, March 25, 2014

ARSENAL YAWASAFISHA NYOTA WAKE KUFUATIA KADI NYEKUNDU YENYE UTATA.

KLABU ya Arsenal imefanikiwa kuhakikisha kuwa hakuna mchezaji yoyote kati ya Kieran Gibbs au Alex Oxlade-Chamberlain aliyeadhibiwa kufuatia kadi nyekundu yenye utata ilitolewa Jumamosi katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Chelsea. Gibbs alitolewa nje na mwamuzi Andre Marriner badala ya Oxlade-Chamberlain ambaye alishika mpira uliopigwa na Eden Hazard. Chama cha Soka cha Uingereza-FA kilibadilisha kadi nyekundu hiyo na kupatia Oxlade-Chamberlain lakini Arsenal walifanikiwa kushawishi jopo lililokuwa likisikiliza shauri hilo wakiwa kuwa mchezaji hazuia bao kufungwa kwasababu mpira ulikuwa ukielekea nje. Mwamuzi huyo naye pia aliepuka adhabu ambapo yeye pamoja na wasaidizi wake wiki watachezesha mchezo mwingine wa Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment