Wednesday, March 26, 2014

BAYERN WAWEKA REKODI KWA KUBEBA SAHANI YA BUNGESLIGA MAPEMA ZAIDI.

KLABU ya Bayern Munich wametawadhwa kuwa mabingwa wa soka wa Ujerumani kwa mara ya 24 huku wakiweka rekodi ya kunyakuwa taji hilo wakiwa wamebaki na mechi saba. Ubingwa huo umekuja kufuatia ushindi wa mabao 3-1 waliopata ugenini dhidi ya Hertha Berlin mabao ambayo yalifungwa na kiungo Tony Kroos, Mario Gotze na Franck Ribery. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Guardiola amesema amafurahi kuleta taji lingine muhimu katika klabu hiyo na kuishukuru kwa kumpa nafasi kuwafundisha wachezaji mahiri kama hao. Akiwa tayari ameshanyakuwa taji la tatu katika kipindi kifupi likiwepo la UEFA Super Cup na Klabu Bingwa ya Dunia, Guardiola sasa anaweza kuhamishia nguvu zake kuhakikisha wanatetea taji la Ulaya walilopata mwaka jana.

No comments:

Post a Comment