Tuesday, March 25, 2014

BECKHAM KUJENGA BONGE LA UWANJA MIAMI.

NAHODHA wa zamani wa Uingereza, David Beckham amebainisha mpango wake wa kujenga uwanja wenye uwezo kubeba mashabiki 25,000 karibu na ufukwe jijini Miami kwa ajili ya timu yake anayotaka kuanzisha. Beckham mwenye umri wa miaka 38 alistaafu soka Mei mwaka jana na mapema mwaka huu alitangaza mpango wake wa kuanzisha timu itakayoshiriki Ligi Kuu nchini Marekani-MLS kutoka katika jiji hilo. Beckham amesema watu wanapofikiria Miami haraka wanafikiria kuwa karibu na maji ndio maana amemua kuweka uwanjani huo karibu na maji. Uwanja huo wa wazi utakuwa karibu na uwanja wa timu ya mpira wa kikapu ya Miami heat.

No comments:

Post a Comment