Friday, March 7, 2014

BILIONEA WA KLABU YA BIRMINGHAM AHUKUMIWA JELA MIAKA SITA.

MMILIKI wa klabu ya Birmingham City Carson Yeung amehukumiwa jela miaka sita na mahakama ya Hong Kong baada ya kukutwa na hatia ya kutakatisha fedha chafu. Yeung mwenye umri wa miaka 54 alihukumiwa Jumatatu kwa makosa matano yanayohusu paundi milioni 55 zilizopitia katika akaunti yake kati ya mwaka 2001 hadi 2007. Bilionea huyo alishitakiwa mwaka 2011 ikiwa ni miaka miwili toka ainunue Birmingham. Yeung ambaye ni mtengeneza mitindo ya nywele ameai kuwa amejipatia utajiri wake kupitia biashara ya hisa, kukodisha majumba, saluni za kutengeneza nywele na kamari.

No comments:

Post a Comment