Friday, March 7, 2014

WILSHERE HATI HATI KOMBE LA DUNIA.

KIUNGO wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Arsenal, Jack Wilshere yuko katika hatihati ya kukosa michuano ya Kombe la Dunia kufuatia ya klabu yake kuwa majeraha ya mguu yanayomkabili yanaweza kumuweka nje kwa zaidi ya wiki tisa. Mguu wa kiungo huyo unatarajiwa kupona kwa muda wa wiki sita na klabu yake inategemea inategemea kwamba anaweza kurejea rasmi baada ya wiki tatu au zaidi. Majeruhi hayo yatamfanya Wilshere kukosekana katika kikosi cha Arsenal mpaka wiki ya pili ya mwezi Mei mwaka huu hivyo kukosa mbio za timu kujaribu kukata kiu ya miaka tisa ya kukosa mataji. Kiungo alipata majeraha hayo baada ya kukwatuliwa na beki wa Denmark Daniel Agger katika mchezo wa kirafiki baina ya timu hizo uliochezwa katika Uwanja wa Wembley ambapo Uingereza ilishinda kwa bao 1-0.

No comments:

Post a Comment