Monday, March 31, 2014

FELLAINI AKWEPA ADHABU.

KIUNGO wa klabu ya Manchester United Marouane Fellaini hatapewa adhabu yoyote kutoka Chama cha Soka cha Uingereza-FA juu ya tuhuma za kumtemea mchezaji mwenzake mate. Fellaini alionekana katika picha za video akisimama juu ya beki wa Manchester City Pablo Zabaleta katika mchezo kati ya timu hizo uliochezwa wiki iliyopita na alikuwa katika hatari ya kufungiwa mechi tatu. Hata hivyo hofu hiyo imeondoka baada ya United kuhabalishwa kuwa Mbeligiji huyo ahatapewa adhabu yoyote. Katika taarifa yake FA ambayo ilikuwa imetaka picha zaidi za video kuchunguza tukio hilo, imedai kuwa hana kosa la kujibu kwasababu hakufanya tukio lolote baya kama ilivyodhaniwa.

No comments:

Post a Comment