Friday, March 28, 2014

GIGGS NA NYOTA WENZAKE WA "CLASS OF 92" WAJIPANGA KUNUNUA TIMU.

RYAN Giggs na wachezaji wengine wanne wa zamani wa Manchester United wamekubaliana na mpango wa kununua timu isiyoshiriki ligi yoyote ya Salford City. Giggs akiwa katika msimu wake wa 24 kama mchezaji Old Trafford ameungana na wachezaji wengine wakiwemo ndugu wawili Gary na Phil Neville, Paul Scholes na Nicky Butt. Giggs mwenye umri wa miaka 40 ambaye kwasasa ni kocha mchezaji wa United amesema wanataka kutumia uzoefu na weledi wao katika soka kusaidia vijana wadogo ambao wanachipukia. Nyota hao hivi sasa wanasubiri Chama Cha Soka cha Uingereza-FA kupitisha mpango wao huo wa kuinunua timu hiyo.

No comments:

Post a Comment