Friday, March 28, 2014

WILLIAMS ATINGA FAINALI SONY OPEN.

MWANADADA nyota wa tenisi kutoka Marekani, Serena Williams ameendeleza rekodi yake ya kushinda mechi 15 mfululizo dhidi ya Maria Sharapova wa Urusi na kutinga fainali yake ya tisa ya michuano ya wazi ya Sony inayofanyika huko Miami. Williams anayeshika namba moja katika orodha za ubora duniani alifanikiwa kumgaragaza Sharapova kwa 6-4 6-3. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Williams amesema haikuwa kazi rahisi kwasababu mpinzani wake alikuwa akifanya vyema hivyo ilibidi atumie nguvu ili kufanya vizuri zaidi na kuweza kushinda mchezo huo. Williams ambaye ameshinda mara sita taji la michuano hiyo sasa atakwaana na aidha Dominika Cibulkova wa Slovakia au Li Na wa China.

No comments:

Post a Comment