Friday, March 28, 2014

HENRY KUKUTANA NA WENGER JULAI.

NAHODHA wa timu ya New York Red Bulls ya Marekani, Thierry Henry amekiri kuwa litakuwa jambo la ajabu kwake kucheza dhidi ya klabu yake ya zamani ya Arsenal wakati watakapofanya ziara Julai mwaka huu. Arsenal na Red Bulls walithibitisha jana kuwa watacheza mechi ya kirafiki Julai 26 ikiwa ni sehemu ya ziara ya klabu hiyo nchini humo. Mechi hiyo itakuwa mahsusi kwa Arsenal kujiandaa na msimu wa 2014-2015 wa Ligi Kuu na Henry ambaye amecheza mechi 254 akiwa na timu hiyo kuanzia mwaka 1999 na 2007 anajua kuwa itakuwa fikra tofauti kucheza na timu yake hiyo ya zamani. Henry amesema mara zote anapocheza dhidi ya Arsenal linakuwa jambo la ajabu kwake, alishawahi kufanya hivyo akiwa na Barcelona walipoenda kucheza michuano ya Kombe la Emirates na sasa wanakuja tena akiwa Marekani.


No comments:

Post a Comment