Sunday, March 30, 2014

KIPIGO DHIDI YA CRYSTAL PALACE KIMETUNYIMA UBINGWA - MOURINHO.

MENEJA wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho anaamini kuwa kipigo walichopata kutoka kwa Crystal Palace kimewaondolea nafasi ya kunyakuwa taji la Ligi Kuu msimu huu.  Bao pekee la kujifunga lililowekwa wavuni na nahodha John terry lilitosha kuihakikishia ushindi wa bao 1-0 Palace katika Uwanja wa Selhurst Park. Ingawa bado wanaendelea kukaa kuongoza ligi kwa tofauti ya alama moja lakini wanaweza kupitwa na iadha Liverpool au Manchester City kama wakishinda mechi zao za mkononi ambazo hawajacheza. Mourinho amesema matokeo hayo yameondoa matumaini yao ya kuendelea kukaa kileleni kwasababu wanategemea zaidi ya wenzao ambao wanawafukuzia kwasasa.

No comments:

Post a Comment