Saturday, March 22, 2014

MOURINHO ALALAMIKIA FA KUTOMTENDEA HAKI.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amedai kuwa Chama cha Soka cha Uingereza-FA, huwa kinamfanyia visivyo baada ya kushitakiwa kwa tabia zisizo za kiungwana kwa kufukuzwa katika benchi lake la ufundi katika mchezo dhidi ya Aston Villa. Mourinho alitolewa baada ya kuingia uwanjani kuzungumza na mwamuzi Chris Foy akipinga kutolea nje kwa kadi nyekundu kwa Ramires ambapo Chelsea iliambulia kipigo cha bao 1-0 katika Uwanjwa Villa Park. Wakati Mourinho akiwa tayari amebainisha kukata rufani kuhusiana na suala hilo amebainisha pia anavyochanganyikiwa na jinsi FA wanavyomfanyia. Mourinho amesema pamoja na kutendewa ndivyo sivyo lakini bado anaendelea kuwa na imani ya juu kwa waamuzi wa Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment