Thursday, March 27, 2014

NAJISIKIA NYUMBANI NIKICHEZA SAMBAMBA NA PIRLO - TEVEZ.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Juventus, Carlos Tevez amesema anajisikia kuwa nyumbani akiwa katika kikosi hicho sambamba na kiungo Andrea Pirlo. Tevez ambaye alijiunga na Juventus akitokea klabu ya Manchester City, ameendeleza wimbi lake la upachikaji mabao akiwa amefunga mabao 19 katika mshindano yote mpaka sasa. Nyota huyo amesema anajisikia vyema kuwemo katika kikosi cha Juventus chini ya kocha Antonio Conte pamoja na wachezaji wenzake akiwemo mkongwe Pirlo. Conte amekigeuza kikosi cha Juventus kuwa cha ushindi na siku zote amekuwata nyota wake kufanya vizuri ndani na nje ya uwanja.

No comments:

Post a Comment