Sunday, March 30, 2014

REUS ATUMA SALAMU SANTIAGO BERNABEU.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Ujerumani, Marco Reus amewaonya Real Madrid kuwa klabu yake ya Borussia Dortmund wako tayari kwa ajili ya mchezo war obo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Jumatano. Dortmund wamejiweka vyema kwa ajili ya safari yao ya kwenda Hispania kwa ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya timu iliyo katika hatari ya kushuka daraja ya Stuttgart huku Reus akifunga mabao matatu-hat trick. Reus anaamini kiwango alichoonyesha katika mchezo huo ni dalili tosha kwamba amerudi baada ya kusumbuliwa na majeruhi Machi mwaka huu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 amesema mabao aliyofunga ni muhimu kwani yamewaongezea kujiamini zaidi na sasa wako tayari kwa ajili ya Madrid.

No comments:

Post a Comment