Sunday, March 30, 2014

VITALY KLITSCHKO AJITOA KINYANG'ANYIRO CHA URAIS UKRAINE.

MWANASIASA maarufu na bondia wa zamani nchini Ukraine, Vitaly Klitschko amejitoa katika kinyang’anyiro cha mbio za urais nchini humo zilizopangwa kufanyika Mei mwaka huu. Bingwa huyo wa dunia wa mwasumbwi ya uzito wa juu amesema badala yake atamuunga mkono mwanasiasa tajiri Petro Poroshenko katika uchaguzi huo. Wote wawili walikuwa sehemu muhimu ya maandamano mtaani ambayo yalipelekea kung’olewa kwa aliyekuwa rais wan chi hiyo Voktor Yanukovych. Kujitoa kwa Klitschko kunamaanisha kuwa mbio za urais sasa zitakuwa kati ya Poroshenko na aliyekuwa Waziri Mkuu Yulia Tymoshenko ambaye aliyotolewa gerezani hivi karibuni baada ya kuangushwa kwa utawala wa Yanukovych.

No comments:

Post a Comment