Monday, March 31, 2014

SITAHARAKISHA KUPONA GOTI LANGU - FALCAO.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Colombia, Radamel Falcao amedai kuwa pamoja na kwamba anaendelea vyema kupona kutokana na majeruhi ya goti, hatachukua maamuzi yoyote ya hatari kwa ajili ya kucheza michuano ya Kombe la dunia baadae mwaka huu. Falcao mwenye umri wa miaka 28 aliumia vibaya goti lake wakati akiitumikia klabu yake ya Monaco Januari mwaka huu na mshambuliaji huyo amesema hataharakisha kupona kwake. Nyota huyo amesema ni jambo lililo wazi kuwa anatamani kupona haraka ili aweze kuiwakilisha nchi yake katika michuano ya Kombe la Dunia lakini hataki jambo hilo limuathiri

No comments:

Post a Comment